current location : Lyricf.com
/
Songs
/
Nimekubali lyrics
Nimekubali lyrics
turnover time:2024-06-23 15:07:10
Nimekubali lyrics

Kapipo on the beat, hey eeeh

Ooh nanana, ooh mamama

Maulana mmmh

(Kapipo)

Kapu limeshajaa

Mapitilizo maudhi yamezidi

Moyo wangu uko mbali nawe

Soko la karafuu umeuza dagaa

Na ule utamu umeugawia kijiji

Umenipa donda la roho

Isipagawe

Mungu amenipa ufahamu

Natambua lipi chema na baya

Usizuge kwa tabasamu

Kumbe huna lako moyoni

Na nishazoea mila

Kikwetu kusema sema ni roho mbaya

Ningalikuwa na uwezo

Mwanzo ningekuficha mfukoni

Ulinidanganya kumbi kumbi

Nilale bila chandarua

Kumbe mbu nang'ata

Si ulinikung'uta mavumbi

Nilipo omba nyingi dua

Ukaniondolea mashaka

Mapenzi hayalazimishwi

Haukuridhiana na mimi nenda

Ila nakuombea

Ukaishi maisha mema

Pia siwezi na silazimishi

Labda sina dhamani, huenda

Kuondoka kwako kwangu

Mungu akaleta mema

Nimekubali mimi, japo ni maumivu ila

Nimekubali mimi, japo hutoki kwa akili yangu unaizunguka

Nimekubali mimi, nimekubaliana na wewe eeh

Nimekubali mimi, nimekubaliana na weee

Japo ni ngumu ka imenikwama miiba

Maana kwa ndani ndani bado inanichoma

Na maumivu huwezi yasikia

Nayasikia mwenyewe tu

Na hali ya upweke sio kawaida

Najua dhahiri kuwa na kinyima amani

Stress ingekuwa kilevi

Ndio kulala na viatu

Jua mwana ukiyataka ndo mwana kuyapata

Mungu hamnyimi mja wake

Usinung'unike kwa utakacho kipata

Maana ndo unachotafuta

Umekuwa gari la taka, haunaga tabaka

Umekosa hadhi ya mwanamke

Tulia yakufuate magari bovu

Ndo kutwa ukafuata fuata wee

Mapenzi hayalazimishwi

Haukuridhiana na mimi nenda

Ila nakuombea

Ukaishi maisha mema

Pia siwezi na silazimishi

Labda sina dhamani, huenda

Kuondoka kwako kwangu

Mungu akaleta mema

Nimekubali mimi, japo ni maumivu ila

Nimekubali mimi, japo hutoki kwa akili yangu unaizunguka

Nimekubali mimi, nimekubaliana na wewe eeh

Nimekubali mimi, nimekubaliana na weee

Ibraah, Konde music worldwide

(And the good music has been done by Kapipo)

Comments
Welcome to Lyricf comments! Please keep conversations courteous and on-topic. To fosterproductive and respectful conversations, you may see comments from our Community Managers.
Sign up to post
Sort by
Show More Comments
Ibraah
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili, English
Ibraah
Latest update
Copyright 2023-2024 - www.lyricf.com All Rights Reserved