current location : Lyricf.com
/
Songs
/
Tukaze Roho lyrics
Tukaze Roho lyrics
turnover time:2024-07-02 05:18:24
Tukaze Roho lyrics

Spice music

Maisha yangu si ya ki papa

Ni vitembele ya nyanya chungu

Dagaa kurusungu, hummh

Niko chakavu na nimechakaa

Yaani naishi ki mungu mungu

Mtetezi wa bunjuu

Mjukuu wa binti simba

Okoa mangala

Wa mwisho kitinda mimba

Mwenye elimu uchwara

Maisha yalivyo nifilimba, akanijalia jallah

Nikaanza kuimba, uniondoke ufukara

Ila bado,

Kipato changu cha chini nacho kina utata

Hata visenti hamsini kuvipata mashaka

Nalia na umasikini mungu ashushe baraka

Enyi wezangu na mimi tusikate tamaa

Tukaze roho, tukaze roho tusichoke

Tukaze roho ,mungu wa kwetu sote

Tukaze roho, eeh tusichoke

Tukaze roho, mungu wa kwetu sote

Mmh

Japo, maisha yenye ya manati

Hatupati kila tukilenga

Kukicha misumari ya bati

Kuku kapenya kwa tenga

Kula yetu tu ni wasiwasi

Tutapata wapi ya kujenga

Wa kupiga picha masaai

Kulala mbagala kwa chemba

Tunaunga unga mwana (haya ndo mambo yetu)

Hayana tofauti na jana (ndo maisha yetu)

Wazazi kulala na mwana (heey...)

Chumba kimoja mandoo, masufuria (wenyewe tushazoea)

Kipato changu cha chini, nacho kina utata

Ata visenti hamsini kuvipata mashaka

Nalia na umasikini mungu ashushe baraka

Enyi wezangu na mimi tusikate tamaa

Tukaze roho, tukaze roho tusichoke

Tukaze roho, mungu wa kwetu sote

Tukaze roho, eeh tusichoke

Tukaze roho, mungu wa kwetu sote

(Ayolizer)

Wanangu wa bodaboda, tukaze roho

Kina mama vikoba, tukaze roho

Ah rumbesi wabeba virogha, tukaze roho

Vijana wezangu, tukaze roho

Tutapata tu

Comments
Welcome to Lyricf comments! Please keep conversations courteous and on-topic. To fosterproductive and respectful conversations, you may see comments from our Community Managers.
Sign up to post
Sort by
Show More Comments
Lava Lava
  • country:Tanzania
  • Languages:Swahili
Lava Lava
Latest update
Copyright 2023-2024 - www.lyricf.com All Rights Reserved